• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Complaints |
    • Gms |
SHIRIKA LA MASOKO YA KARIAKOO
SHIRIKA LA MASOKO YA KARIAKOO

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania OFISI YA RAIS TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA SHIRIKA LA MASOKO YA KARIAKOO

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Dhima
    • Muundo wa Taasisi
    • Majukumu ya msingi
  • Utawala
    • Idara
      • Human Resources and Administration
      • Health and Sanitation
      • Finance
      • Planning and Commercial
    • Vitengo
      • Maintenance Service
      • Internal Audit
      • Procurement Management
      • Information and Communication Technologies
      • Legal Services
      • Security
  • Kituo cha habari
    • Habari
    • Matangazo
    • Maktaba ya picha
    • Press-Releases
    • Video
  • Marketing
    • Products and Services
    • Marketing Price
  • Miradi na Fursa za uwekezaji
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Fursa za Uwekezaji
  • Manunuzi
    • Zabuni
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Fomu
    • Journals/Newsletter
    • Reports
    • Hotuba
  • Huduma mtandao
    • Revenue Collection(TAUSI)
    • GISP Portal
    • Employees Self Service Portal
    • E - Mrejesho
    • E - Board
    • E - Mikutano

Maafisa Habari Toeni Ufafanuzi Dhidi ya Upotoshaji - Mchengerwa

Posted on: May 24th, 2025

Na.Revocatus Kassimba

Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais - TAMISEMI, Mohamed Mchengerwa, amewataka Maafisa Habari kujitokeza hadharani kujibu na kutoa ufafanuzi sahihi kuhusu maendeleo yanayofanywa na Serikali, hususan pale ambapo upotoshaji wa makusudi unapotokea. 


Akifungua kikao kazi cha Maafisa Habari wa Mikoa, Halmashauri, na Taasisi za Ofisi ya Rais - TAMISEMI kilichofanyika Dodoma Mei 23, 2025, Mchengerwa aliwakumbusha wajibu wao wa kuzungumza ukweli kuhusu mafanikio ya Serikali ya Awamu ya Sita chini ya uongozi wa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan.


Mchengerwa alionya dhidi ya kuwaruhusu Watanzania kuzoea kulishwa taarifa potofu na watu wenye nia mbaya hivyo aliwataka Maafisa Habari kwenda kutoa habari sahihi na kueleza mazuri yanayofanywa na Serikali.


“Tusiwafanye watanzania kuzoea kulishwa taarifa potofu, nendeni mkatoe ufafanuzi na habari sahihi ikiwemo kuzungumzia mazuri yanayiendelea Tanzania” alisisitiza Mchengerwa.


Mchengerwa alitaja kuwa bajeti ya TAMISEMI kwa mwaka 2025/26 ni Trilioni 11.7, ambayo ni asilimia 21 ya bajeti yote yq Serikali hivyo, alihimiza Maafisa Habari kuitangaza na kuisemea miradi hiyo kwenye vyombo vya habari .


Kwa upande wake Kaimu Katibu Mkuu OR-TAMISEMI, Mhandisi Novatus Mativila, aliwataka Maafisa Habari kufanya kazi kwa juhudi na ubunifu huku wakizingatia wakati uliopo.


Akiwasilisha mada Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Utangazaji Tanzania (TBC), Dkt. Ayub Rioba, alihimiza Maafisa Habari kuongeza ubunifu katika kazi zao, ikiwemo kutumia mitandao ya kijamii na redio. 


Dkt.Rioba alisema kuwa kufanya hivyo kutasaidia kufikisha maudhui bora kwa jamii, hatua ambayo itachangia wananchi kutambua shughuli za Serikali na kuendelea kuiunga mkono.


Mwisho.

Matangazo

  • Taarifa kwa Umma January 31, 2025
  • Taarifa kwa Umma January 29, 2025
  • Usajili wa wafanyabiashara November 14, 2023
  • Tangazo la Uchaguzi wa Serikali za Mitaa 2024 August 15, 2024
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • SHIRIKA LA MASOKO YA KARIAKOO, SHIRIKA LA UZALISHAJI MALI JESHI LA POLISI WAKUTANA KUJADILI MIKAKATI YA ULINZI SOKO LA KARIAKOO.

    January 09, 2026
  • WATUMISHI WA WASHIRIKA LA MASOKO WAJENGEWA UWEZO MATUMIZI YA E-MREJESHO.

    January 08, 2026
  • SOKO LA KARIAKOO LATENGA VYUMBA MAALUM VYAA KUNYONYESHA KWA WAKINA MAMA.

    December 30, 2025
  • UKARABATI NA UJENZI WA SOKO LA KARIAKOO WAFIKIA ASILIMIA 99, TAYARI KWA KUFUNGULIWA.

    December 24, 2025
  • Angalia zote

Video

Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • TAMISEMI
  • eGovernment Authority
  • Employees Self Service Portal

Viunganishi Linganifu

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana nasi

Other Contacts

   

Visitors Counter

www.freevisitorcounters.com

    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti
    • Huduma

Copyright ©2024 Shirika la Masoko ya Kariakoo . All rights reserved.