• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Complaints |
    • Gms |
SHIRIKA LA MASOKO YA KARIAKOO
SHIRIKA LA MASOKO YA KARIAKOO

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania OFISI YA RAIS TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA SHIRIKA LA MASOKO YA KARIAKOO

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Dhima
    • Muundo wa Taasisi
    • Majukumu ya msingi
  • Utawala
    • Idara
      • Human Resources and Administration
      • Health and Sanitation
      • Finance
      • Planning and Commercial
    • Vitengo
      • Maintenance Service
      • Internal Audit
      • Procurement Management
      • Information and Communication Technologies
      • Legal Services
      • Security
  • Kituo cha habari
    • Habari
    • Matangazo
    • Maktaba ya picha
    • Press-Releases
    • Video
  • Marketing
    • Products and Services
    • Marketing Price
  • Miradi na Fursa za uwekezaji
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Fursa za Uwekezaji
  • Manunuzi
    • Zabuni
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Fomu
    • Journals/Newsletter
    • Reports
    • Hotuba
  • Huduma mtandao
    • Revenue Collection(TAUSI)
    • GISP Portal
    • Employees Self Service Portal
    • E - Mrejesho
    • E - Board
    • E - Mikutano

Mafunzo ya Afya kwa Watumishi Soko la Kariakoo

Posted on: May 10th, 2025

Mkurugenzi Mtendaji wa Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH), Prof. Mohamed Janabi, amewataka watumishi wa Shirika la Masoko ya Kariakoo kujenga utamaduni wa kupima afya angalau mara moja kwa mwaka.

Alisema hatua hiyo itasaidia kutambua mapema dalili za magonjwa sugu yasiyoambukiza na hivyo kupata tiba kwa wakati, kuepusha athari zinazoweza kupunguza nguvu kazi ya taifa.

Prof. Janabi alitoa ushauri huo alipokuwa akizungumza wakati wa mafunzo ya siku moja kwa watumishi wa shirika hilo yaliyofanyika katika Hospitali ya Taifa Muhimbili ( Mei 9, 2025).

Katika mada yake kuhusu ugonjwa wa kiarusi, alieleza kuwa mtindo mbaya wa maisha, shinikizo la juu la damu, unywaji pombe kupita kiasi, na ulaji wa vyakula vyenye sukari na mafuta mengi ni sababu kuu zinazochangia ugonjwa huo.

"Ni muhimu kufanya uchunguzi wa afya zenu kila mwaka ili kuepuka kugundua magonjwa mkiwa katika hatua za mwisho au uzeeni, hali ambayo inaweza kusababisha madhara makubwa kwa afya zenu," alisisitiza Prof. Janabi ambaye ni mtaalamu bingwa wa magonjwa ya moyo.

 Prof.Janabi aliongeza kuwa dunia inakabiliwa na magonjwa mengi hatari kama vile moyo, shinikizo la damu, kisukari, figo, na kiarusi, ambayo yanasababisha vifo vingi. Hivyo, upimaji wa afya wa mapema ni muhimu ili kujua dalili na kupata matibabu stahiki.

Meneja Mkuu wa Shirika la Masoko ya Kariakoo, CPA. Ashraph Abdulkarim, alieleza kuwa shirika limeandaa mafunzo hayo kama sehemu ya mkakati wa kuwajengea uwezo watumishi wake ili waweze kufahamu hali zao za afya na kuchukua hatua za mapema kudhibiti magonjwa.

CPA Abdulkarim alishukuru Hospitali ya Taifa ya Muhimbili kwa kutoa mafunzo kwa watumishi 35 ambao wana jukumu muhimu la kuhudumia wafanyabiashara na wananchi katika soko hilo.

Katika mada nyingine, Dkt. Garvin Kweka aliwaasa watumishi kuwa waaminifu kwa wenzi wao na kuchukua tahadhari dhidi ya maambukizi ya VVU/UKIMWI kwa kuepuka ngono zembe na matumizi mabaya ya vileo.

Naye Afisa Mwelimishaji kutoka Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) mkoa wa Ilala, Bi. Mary Mwakyusa, aliwaonya watumishi dhidi ya vitendo vya rushwa wanapohudumia wafanyabiashara wa Soko la Kariakoo.

Matangazo

  • Taarifa kwa Umma January 31, 2025
  • Taarifa kwa Umma January 29, 2025
  • Usajili wa wafanyabiashara November 14, 2023
  • Tangazo la Uchaguzi wa Serikali za Mitaa 2024 August 15, 2024
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • SHIRIKA LA MASOKO YA KARIAKOO, SHIRIKA LA UZALISHAJI MALI JESHI LA POLISI WAKUTANA KUJADILI MIKAKATI YA ULINZI SOKO LA KARIAKOO.

    January 09, 2026
  • WATUMISHI WA WASHIRIKA LA MASOKO WAJENGEWA UWEZO MATUMIZI YA E-MREJESHO.

    January 08, 2026
  • SOKO LA KARIAKOO LATENGA VYUMBA MAALUM VYAA KUNYONYESHA KWA WAKINA MAMA.

    December 30, 2025
  • UKARABATI NA UJENZI WA SOKO LA KARIAKOO WAFIKIA ASILIMIA 99, TAYARI KWA KUFUNGULIWA.

    December 24, 2025
  • Angalia zote

Video

Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • TAMISEMI
  • eGovernment Authority
  • Employees Self Service Portal

Viunganishi Linganifu

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana nasi

Other Contacts

   

Visitors Counter

www.freevisitorcounters.com

    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti
    • Huduma

Copyright ©2024 Shirika la Masoko ya Kariakoo . All rights reserved.