• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Complaints |
    • Gms |
SHIRIKA LA MASOKO YA KARIAKOO
SHIRIKA LA MASOKO YA KARIAKOO

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania OFISI YA RAIS TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA SHIRIKA LA MASOKO YA KARIAKOO

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Dhima
    • Muundo wa Taasisi
    • Majukumu ya msingi
  • Utawala
    • Idara
      • Human Resources and Administration
      • Health and Sanitation
      • Finance
      • Planning and Commercial
    • Vitengo
      • Maintenance Service
      • Internal Audit
      • Procurement Management
      • Information and Communication Technologies
      • Legal Services
      • Security
  • Kituo cha habari
    • Habari
    • Matangazo
    • Maktaba ya picha
    • Press-Releases
    • Video
  • Marketing
    • Products and Services
    • Marketing Price
  • Miradi na Fursa za uwekezaji
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Fursa za Uwekezaji
  • Manunuzi
    • Zabuni
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Fomu
    • Journals/Newsletter
    • Reports
    • Hotuba
  • Huduma mtandao
    • Revenue Collection(TAUSI)
    • GISP Portal
    • Employees Self Service Portal
    • E - Mrejesho
    • E - Board
    • E - Mikutano

UKARABATI NA UJENZI WA SOKO LA KARIAKOO WAFIKIA ASILIMIA 99, TAYARI KWA KUFUNGULIWA.

Posted on: December 24th, 2025

UKARABATI NA UJENZI WA SOKO LA KARIAKOO WAFIKIA ASILIMIA 99, TAYARI KWA KUFUNGULIWA.

 

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (OWM-TAMISEMI), Mhe. Prof. Riziki Shemdoe ameupongeza uongozi wa Shirika la Masoko Kariakoo kwa kushirikiana na Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam kwa namna lilivyoratibu zoezi la kuwarudisha wafanyabiashara 1520 waliokuwepo sokoni hapo kabla ya soko hilo kuungua mwaka 2021.


Prof. Shemdoe ametoa pongezi hizo leo, alipofanya ziara katika soko la Kariakoo, ziara ambayo ilikuwa na lengo kukagua maendelea ya ukarabati na ujenzi wa soko hilo la kimataifa na Kongwe hapa nchini.


Prof. Shemdoe ameongeza kuwa uwepo wa soko hilo kumechochea sekta binafsi kuongeza kasi ya uwekezaji wa majengo ya biashara mbalimbali ambayo yameongeza kasi ya upatikanaji wa ajira kwa wananchi ikiwemo vijana na hivyo kufangamanisha sekta ya ummaa na binafsi.


“Nimetembelea soko hili, nimeridhika kwa namna ujenzi huu ulivyofanyika, naishukuru sana Serikali ya Awamu Sita kwa kutoa Bilioni 28 ambazo zimetumika kukarabati na kujenga upya soko hili ambalo lilipata ajali ya moto mwaka 2021” amesema Prof. Shemdoe


Kwa upande wake Katibu Tawala Msaidizi Miundombinu Mkoa wa Dar es Salaam, Mhandisi Amani Mafuru amesema ujenzi na ukarabati wa soko hilo umekamilika kwa asilimia 99 ambapo ujenzi huo umejumuisha kuweka miundombinu ya kudhibiti moto, miundombinu kwa ajili ya watu wenye mahitaji maalum na kuwepo kwa lift za kubebea watu na mizigo kitu kinachofanya soko hilo kuwa la kisasa zaidi.


Naye Kaimu Meneja Mkuu wa Shirika la Masoko Kariakoo, Bi. Mwinga Luhoyo amesema zoezi la kuwapangia wafanyabiashara maeneo lilikuwa ni shirikishi ambapo viongozi wa wafanyabiashara hao walishirikishwa, miongoni mwao wameshajaza mikataba na tayari imeshaingizwa kwenye mfumo wa TAUSI tayari kwa kuanza biashara soko litakapofunguliwa.


Matangazo

  • Taarifa kwa Umma January 31, 2025
  • Taarifa kwa Umma January 29, 2025
  • Usajili wa wafanyabiashara November 14, 2023
  • Tangazo la Uchaguzi wa Serikali za Mitaa 2024 August 15, 2024
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UKARABATI NA UJENZI WA SOKO LA KARIAKOO WAFIKIA ASILIMIA 99, TAYARI KWA KUFUNGULIWA.

    December 24, 2025
  • WATUMISHI KARIAKOO WAPEWA MKONO WA SIKUKUU ZA MWISHO WA MWAKA, WAHIMIZWA KUENDELEA KUWAJIBIKA.

    December 22, 2025
  • SOKO LA KARIAKOO MBIONI KUFUNGULIWA

    December 19, 2025
  • SHIRIKA LA MASOKO YA KARIAKOO LAANZA KUANDAA MPANGO MKAKATI WA MIAKA MITANO 2026-2031.

    December 12, 2025
  • Angalia zote

Video

Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • TAMISEMI
  • eGovernment Authority
  • Employees Self Service Portal

Viunganishi Linganifu

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana nasi

    General Manager, Kariakoo Markets Corporation, Nyamwezi/Tandamti Street,

    Anuani ya posta: P. O. Box 15789 Dar es Salaam, Tanzania

    Simu: +255 22 2180678

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe za Watumishi: info@kariakoomarket.co.tz

Other Contacts

   

Visitors Counter

www.freevisitorcounters.com

    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti
    • Huduma

Copyright ©2024 Shirika la Masoko ya Kariakoo . All rights reserved.